Bondia wa Marekani Deontay Wilder amelaumu vazi alilovaa na kuingia nalo ndani ya ulingo wa ndondi kama sababu iliomfanya kupoteza taji lake la WBC katika uzani mzito zaidi duniani kwa Muingereza Tyson Fury.
Raia huyo wa Marekani mwenye umri wa miaka 34 alisema kwamba vazi hilo lilikuwa zito sana hatua iliomfanya kukosa nguvu miguuni katika pigano hilo.
Fury mwenye umri wa miaka 34 alionyesha umahiri wake ili kushinda taji katika mji wa Las Vegas siku ya Jumamosi wakati kona ya Wilder iliposalimu amri kwa kutupa kitambaa cheupe wakati pigano hilo lilipokuwa limefika raundi ya saba.
